• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

FULSA lukuki za Uwekezaji MkoaninRuvuma

Posted on: January 7th, 2022

MKOA wa Ruvuma unatajwa kuwa na fursa lukuki za biashara na uwekezaji katika Halmashauri zote nane ambazo zinawawezesha wawekezaji kuwekeza katika shughuli mbalimbali zinazoweza kuchochea ukuaji wa uchumi.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ib uge amezitaja fursa hizo kuwa zipo katika sekta ya kilimo, biashara, ufugaji,utalii,madini,misitu,mawasiliano,umeme wa maporomoko ya maji,uvuvi,viwanda,uendelezaji wa makazi,usafiri na usafirishaji.

Brigedia Jenerali Ibuge amesema katika Mkoa wa Ruvuma kuna maeneo yanayofaa kwa ujenzi wa viwanda vikubwa,vya kati na vidogo,maeneo ya usambazaji na uuzaji wa bidhaa za viwandani hivyo kuvutia wawekezaji

Kulingana na Mkuu wa Mkoa,maeneo yanayofaa kwa uwekezaji katika sekta kilimo ameyataja kuwa ni  usindikaji wa mazao ya chakula hasa mazao ya tangawizi,mafuta,mbogamboga na matunda.

“Serikali imeendelea na jitihada za kuhakikisha kuwa miundombinu ya barabara na madaraja mkoani Ruvuma inaimarishwa ili kuhakikisha shughuli za usafiri na usafirishaji wa watu na bidhaa mbalimbali kwa ajili ya kuinua uchumi na kupunguza umasikini’’,alisisitiza Ibuge.

Akizungumzia kuhusu meli katika ziwa Nyasa,Brigedia Jenerali Ibuge amesema serikali imenunua meli tatu zinazofanyakazi katika ziwa Nyasa kati hizo meli mbili za mizigo na meli moja ya abiria ambapo meli hizo zinachochea uchumi wa wananchi wanaoishi mwambao mwa ziwa Nyasa na Mkoa wa Ruvuma kwa ujumla.

Kuhusu usafiri wa anga,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amesema serikali kupitia shirika la Ndege ATCL, imeanzisha safari za ndege mpya mara tatu kwa wiki kati ya Songea na mikoa mingine ya jirani.

Amesema kuimarika kwa safari za anga mkoani Ruvuma kuna fungua fursa za biashara na utalii hivyo kuinua uchumi wa wananchi wa Ruvuma na Taifa kwa ujumla

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Januari 7,2022

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa