• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

CMT MADABA WAPATIWA ELIMU NA CRDB KUHUSU MIKOPO NA HUDUMA ZA KIBENKI

Posted on: October 8th, 2025

Wakuu wa Idara wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba mkoani Ruvuma wamepatiwa mafunzo maalumu kutoka Benki ya CRDB kuhusu huduma mbalimbali za kifedha na fursa za mikopo inayotolewa na benki hiyo, katika jitihada za kuongeza uelewa wa watumishi kuhusu masuala ya fedha na maendeleo.

Mafunzo hayo yalifanyika katika Ofisi za Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, yakiongozwa na Meneja wa Kanda ya Kusini wa Benki ya CRDB, Ndg. Denis Mwoleka, ambaye aliambatana na timu ya maofisa wa benki hiyo.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Ndg. Mwoleka alisema lengo kuu ni kuwajengea uwezo watumishi wa umma kuhusu namna bora ya kutumia huduma za benki kwa maendeleo yao binafsi na taasisi wanazozitumikia.

Katika mafunzo hayo, washiriki walipatiwa elimu kuhusu mikopo ya watumishi, mikopo ya wajasiriamali, mikopo ya kilimo, pamoja na mikopo ya vyombo vya usafiri. Aidha, walifundishwa umuhimu wa kuweka akiba kama msingi wa ustawi wa kifedha.

Washiriki walieleza kufurahishwa na mafunzo hayo wakisema yamewapanua uelewa kuhusu fursa zilizopo ndani ya Benki ya CRDB, ambazo zinaweza kuchochea mafanikio ya miradi ya maendeleo ya Halmashauri na wananchi kwa ujumla.

Katika kuadhimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja, Benki ya CRDB pia ilikabidhi keki maalumu kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, ikiwa ni zawadi kwa watumishi wote kama ishara ya upendo, amani, na ushirikiano thabiti kati ya benki hiyo na halmashauri.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • DED MADABA APIGA KURA KATIKA KITUO CHA SHULE YA MSINGI KIFAGURO

    October 29, 2025
  • MAFUNZO YA WASIMAMIZI WA VITUO NA WASIMAMIZI WASAIDI YAFUNGWA RASMI, MSISITIZO WAWEKWA KWENYE UZALENDO NA UADILIFU.

    October 27, 2025
  • WASIMAMIZI WAKUU WA VITUO VYA UCHAGUZI NA WASIMAMIZI WASAIDIZI WAPIGWA MSASA MADABA

    October 26, 2025
  • MKUTANO MKUU WA 32 WA WINO SACCOS WAFANA MADABA

    October 25, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa